Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Odinga asema naye ataapishwa kuiongoza Kenya
Kiongozi wa muungano wa upinzani Kenya wa National Super Alliance Raila Odinga amesema kuwa naye pia ataapishwa kuiongoza Kenya.
Amesisitiza kwamba hamtambui Bw Kenyatta kama rais wa Kenya.
Akihutubia wafuasi wake karibu na uwanja wa Jacaranda ambapo upinzani ulizuiwa kuandaa mkutano, amesema ataapishwa na mabaraza ya wananchi tarehe 12 Desemba.