Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Hamisa: Mwanamke anayewasaidia wanawake wanaowatoroka al-Shabab
Vijana wengi mjini Mombasa wanaotoroka kundi la Al Shabaab kutoka Somalia na kurudi pwani ya Kenya hujikuta hawana la kufanya kwani miongoni mwao watu wao na majirani huwatenga.
Lakini mama Hamisa Maalim Zaja ameamua kuwasaidia hasa wanawake kwa kuwaanzishia biashara mbali mbali.
John Nene amezungumza na Hamisa pamoja na wanawake wanaonufaika kwa mradi wake huo.
Mmoja wao alihadaiwa na ndoa kisha kufika Somalia akawa baadhi ya wanawake wanaowasaidia Al Shabaab na kazi za nyumbani lakini baada ya wiki mbili alipata mwanya na kutoroka pamoja na wenzake wawili