Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mtanziko kwa wanaopata mimba shuleni Tanzania
Suala la mimba za utotoni bado ni kitendawili kikubwa katika nchi za Afrika.
Kwa mujibu wa ripoti ya shirika la Human Rights Watch, nchini Tanzania kuna takriban wasichana 8,000 ambao huacha shule kila mwaka kutokana na kuwa wajawazito.
Na hivi karibuni Rais wa nchi hiyo John Magufuli alipiga marufuku wasichana wenye mimba ama wenye watoto kurudi shule.
Nini hatima ya watoto wa kike?