Ripoti ya mwisho: Ndege ya Malaysia ya MH370 haikupatikana

A message says: "MH370 we miss you"

Chanzo cha picha, AFP/Getty

Maelezo ya picha, Ripoti ya mwisho: Ndege ya Malaysia ya MH370 haikupatikana

Wachunguzi wametoa ripoti yao ya mwisho kuhusu ndege iliyotoweka ya shirika la ndege la Malaysia ikisema kuwa ndege hiyo haikupatikana.

Ndege ya MH370 ilitoweka mwaka 2014 ikiwa safarini kutoka mjini Kuala Lumpur ikienda Beijing ikiwa na abiria 239.

Shughuli ya kuitafuta ndege hiyo iliyohusisha pia China na Malaysia, ilisitishwa mwezi Januari baada ya siku 1,046.

Watafutaji kutoka Australia wanasema kuwa wanajutia sana kuwa ndege hiyo haikupatikana.

Victims' relatives and their supporters protest against the suspension of the search

Chanzo cha picha, AFP/Getty Images

Maelezo ya picha, Familia za wale waliotoweka wametaka shughuli ya kutafuta kurejelewa

Shughuli ya kuitafuta ndege ilikuwa moja ya shughuli kubw zaidi za juu na chini ya habari kuwai kufanywa katika historia ya safari za ndege.

Baada ya shughuli ya siku 52 ya kutafua juu ya habari kukoso kuzaa matunda, wachunguzi walielekea kutafuta kwenye sakafu ya bahari eneo la ukubwa wa kilomita 1200 mraba.

Mwaka 2015-2016 sehemu zilizokisiwa kuwa za ndehe ya MH370 zilisombwa kwenda kwa visiwa vya habari ya Hindi na mashariki pwani ya Afrika Mashariki.