Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mudavadi: Upinzani hauna nia ya kuzua vurugu Kenya
Zimebaki wiki nne kwa raia wa Kenya kurejea tena kwenye uchaguzi. Wakati uchaguzi ukisubiriwa Muungano wa vyama vya upinzani Nasa, umepanga maandamano makubwa hapo Jumanne kushinikiza kuondolewa kwa Afisa Mkuu Mtendaji wa tume ya uchaguzi, Ezra Chiloba na wengine kwa madai ya kuvuruga uchaguzi wa Agosti 8.
Mahakama ya juu kabisa ilifutilia mbali uchaguzi huo kutokana na kugundulika kuwepo na kasoro.
Zuhura Yunus alizungumza na mmoja wa viongozi waandamizi wa NASA Bwana Musalia Mudavadi aliye ziarani London- kwanza akitaka kujua hisia zake baada ya Jubilee kudai kuwa alihusika na udukuzi wakati wa uchaguzi uliopita.