Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mbowe: Madaktari wana matumaini kuhusu Tundu Lissu
Mwenyekiti wa chama cha upinzani Tanzania, Chadema Freeman Mbowe amewaambia wanahabari kwamba madaktari wana matumaini kumhusu Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu ambaye alipigwa risasi Alhamisi mjini Dodoma.
Bw Lissu anaendelea kupokea matibabu alikolazwa mjini Nairobi.
Bw Mbowe, akizungumza na wanahabari Alhamisi jioni alisema mbunge huyo sasa anaweza kula na kuzungumza kidogo.
Mwandishi wa BBC David Wafula na taarifa zaidi.