Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Makataa ya wakimbizi wa Burundi kuondoka Tanzania yakamilika
Serikali za Tanzania na Burundi pamoja na shirika la umoja wa mataifa linalohudumia wakimbizi UNHCR leo watafanya mkutano wa pamoja kuhusiana na kurudishwa kwa wakimbizi wa Burundi waliojiandikisha kurudi kwao kwa hiari.
Pia leo ndio siku ya mwisho ambayo Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania Mwigulu Nchemba aliitoa juu ya utekelezwaji wa zoezi hilo la kuwarudisha wakimbizi hao wa Burundi nyumbani kwao.