Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Uchaguzi Kenya: Nilikimbia nikauacha mkono wangu nyuma
DJ One Hand alikuwa katika mtaa wa Mathare, jijini Nairobi ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 zilipozuka.
Aliona kundi la watu likimzingira mwanamke na akadhamiria kumsaidia mwanamke huyo.
Hakujua kwamba wapo wengine waliokuwa wanamtazama na ghafla alishtukia amekatwa mkono wake mmoja.
Alilazimika kukimbilia usalama wake.
Ana ujumbe gani uchaguzi mkuu Kenya unapokaribia?