Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanawake waliofanywa watumwa wa ngono wa al-Shabab
BBC imewagundua na kuzungumza kwa mara ya kwanza na wanawake Wakenya waliotoroka utumwa wa kingono kutoka kambi za wapiganaji wa Al-Shabab Somalia.
Katika uchunguzi wa kipekee mwandishi Anne Soy amezungumza na kikundi cha wanawake ambao waliathirika na biashara haramu ya binadamu na kusafirishwa hadi Somalia na kunajisiwa.
Tumebadilisha majina yao kwa sababu za usalama wao.