Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ndovu wavamia chuo kikuu cha Dodoma Tanzania
Mara nyingi tumezoea kusikia Tembo wamevamia kijiji au mashamba na kufanya Uharibifu. Jana pia katika Chuo Kikuu cha Dodoma katikati mwa Tanzania walipata ugeni wa tembo wanne wakiwa karibu kabisa na mabweni wanayolala wanafunzi. Lakini ni kweli kuwa mara zote tembo ndio wavamizi?
Kujua hilo, awali nimezungumza na Paschal Shelutete Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA kutaka kujua pia hali ilivyokuwa baada ya tembo hao kuonekana katika eneo hilo.