Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Pacha walioshikana Tanzania walio na ndoto kuu
Ni karibu miongo miwili sasa, tangu mapacha walioungana, Consolata na Maria, walipozaliwa nchini Tanzania.
Mara tu baada ya kuzaliwa, walianza kutunzwa na Kanisa Katoliki, na kujitahidi kuishi maisha ya kawaida, kadri inavyowezekana.
Mwezi huu, wamefikia hatua muhimu sana maishani mwao, kwa kufanya mitihani yao ya mwisho ya sekondari. Mwandishi wetu Leonard Mubali aliwatembelea.