Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Trump alivyomkaribisha mfuasi jukwaani Florida
Rais wa Marekani Donald Trump alimuita na kumkaribisha kwenye jukwaa, mmoja wa wafuasi wake, wakati wa mkutano wake wa hadhara katika jimbo la Florida.
Bw Trump alikuwa akihutubu alipomtambua mmoja wa wafuasi wake kwenye umati ambaye alisema alikuwa amemuona muda mfupi awali kwenye runinga.
Alimpa mfuasi huyo nafasi ya kuhutubia mkutano huo kutoka kwenye jukwaa lake.
Alieleza kwamba alifahamu walinzi wake wa Secret Service hawangefurahishwa na hatua hiyo yake, lakini akasema jambo pekee alilohofia kutoka kwa mfuasi huyo ni kwamba angeweza “kunipiga busu”.