Kanisa takatifu la 'mwujiza wa Yesu' lafunguliwa Israel

Chanzo cha picha, AFP
Misa maalum imefanyika kufungua rasmi kanisa Katoliki Kaskazini mwa Israel ambalo liliteketezwa na Wayahudi wenye itikadi kali mwaka wa 2015.
Kanisa hilo lililoko eneo la Tabgha kando mwa ziwa la Galilee linaaminika na Wakristo kama eneo takatifu ambapo Yesu Kristo alifanya muujiza wa kuwalisha watu 5000 kwa mikate mitano na samaki wawili pekee.
Ukarabati wa kanisa hilo ulichukua miezi minane na kugharimu kima cha dola milioni moja.

Chanzo cha picha, AFP
Licha ya Wayahudi watatu wenye itikadi kali kupatikana na makosa ya kuchoma kanisa hilo hata hivyo hawakuhukumiwa.
Uvamizi huo uliharibu maktaba ya kanisa na jengo nzima.
Hata hivyo sakafu yake iliyotengenezwa karne ya tano ilinusurika uharibifu huo.

Chanzo cha picha, EPA

Chanzo cha picha, AP

Chanzo cha picha, AFP

Chanzo cha picha, EPA









