Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Jamii inayoenzi kitoweo cha mchwa Burundi
Katika nchi nyingi za Afrika wadudu mchwa hupigwa vita na kuuawa kwa dawa mbalimbali za wadudu, lakini huko nchini Burundi, wenyeji wa maeneo ya Buyogoma, Moso na Buragane mpakani na nchi ya Tanzania, mchwa ni kitoweo kwao.
Familia nyingi katika jamii hizo za walaji wa wadudu hao, pia huwafuga na kuwawinda.
Mwenzetu Ismail Misigaro alitembelea eneo la Moso, mashariki mwa Burundi na hii hapa ni taarifa yake.