Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mavazi ya karatasi yampa umaarufu kijana wa Kinshasa
Nguo zilizobuniwa kwa karatasi zimempa umaarufu kijana wa miaka 28, Cedric Mbengi, mjini Kinshasa ambaye amekuwa akizishona na kuuza kwa bei ya hadi dola 500 za Marekani.
Kijana huyu ambaye alikuwa akivaa nguo za bei ghali kama baadhi vijana wengine wa kinshasa wanaojiitaa sapeurs, yeye aliona vyema kuepuka kununua mavazi ya kawaida na kubuni yake ya karatasi.
Amejizolea umaarufu kiasi cha kualikwa hadi maonesho ya ubunifu wa mavazi nchi za Ulaya.
Mwandishi wa BBC Mbelechi Msoshi anaarifu zaidi.