Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwuguzi anayefanya kazi vitani Aleppo, Syria
Um-Yehia hakuwahi kufikiria siku moja atajipata akiishi na kufanya kazi eneo lenye vita mji wa Aleppo.
Alitoroka Homs nchini Syria na kuingia maeneo ya waasi Aleppo baada ya maasi ya 2011.
Alisomea uhasibu, lakini hali ilimlazimu kutafuta njia ya kujikimu.
"Maisha yangu daima yamo hatarini, kelele za ndege hunitia hofu." Kwa hivyo, akawa mwuguzi. Kama mwanamke anayeishi eneo lenye vita, nahisi hospitalini ndipo pahala salama zaidi,” anasema.