Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Pacha walioshikana watenganishwa hospitali ya Kenyatta
Madaktari nchini Kenya wamefanikiwa kufanya upasuaji wa kuwatenganisha pacha walioungana katika sehemu ya chini ya mgongo.
Pacha hao walikuwa hospitalini kwa muda wa miaka miwili tangu walipozaliwa wakingoja upasuaji wa kuwatenganisha.
Walizaliwa mwaka wa 2014 wakiwa na viungo vyote vya mwili isipokuwa sehemu ya chini ya uti wa mgongo ulioshikana na kuwasababisha kutumia njia moja kuenda haja kubwa.
Upasuaji wa aina hiyo kutenganisha sehemu ya uti wa mgongo ndio wa kwanza kufanyika katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara.
Mwandishi wa BBC David Wafula na taarifa zaidi.