Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Utalii: Wadau walalamikia kuongezwa kwa ushuru Tanzania
Watalii nchini Tanzania hivi sasa wanalipa gharama zaidi katika malazi na gharama zingine za kuingia mbugani baada ya ushuru mpya wa VAT kuwekwa. Tanzania inasema asilimia 18 ya ushuru huo wa VAT inahitajika kuiongezea serikali mapato. Utalii unachangia takribani asilimia 14 ya uchumi wa nchi hiyo. Lakini wadau wengi wa utalii wamemwambia Mwandishi wetu Sammy Awami kwamba ushuru huo una madhara katika sekta ya utalii na kwamba biashara zao zimeathirika.