Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kidum ajipata njia panda nchini Burundi
Mwanamuziki mashuhuri wa Burundi mwenye makazi yake nchini Kenya Nimbona Jean Pierre almaarufu Kidum amejikuta matatani akiwa nchini mwake Burundi baada ya kulaumiwa na wapinzani kuwa amekwenda huko kuupigia debe utawala wa Rais Pierre Nkurunziza.
Rasmi, Kidum yuko Burundi kutumbuiza kwenye tamasha ya biashara ilioandaliwa na Ubalozi wa Kenya nchini Burundi.
Lawama dhidi yake zimekuwa nyingi baada ya Kidum kukutana kwa mazungumzo na Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, kiasi ya kupata vitisho huku ulinzi wake ukiimarishwa.
Mwandishi wetu wa Bujumbura, Ramadhani Kibuga amezungumza na Kidum kuhusu tuhuma hizo.