Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwanamke malkia wa urembo gerezani Kenya
Mashindano ya urembo ya idara ya magereza nchini Kenya yalifanyika wiki hii katika jela ya wanawake iliyoko Langata mjini Nairobi.
Washiriki huwa ni wanawake wafungwa pamoja na wale wako rumande, nia kubwa ikiwa ni kuwapa motisha na matumaini ya maisha.
Ruth Kamande aliibuka mshindi akifuatiwa na Tina Martin na Susan Wairimu akawa wa tatu. Wote hao wako rumande.
John Nene amezungumza na Ruth ambaye anakabiliwa na shtaka la mauaji na Tina kutoka Tanzania anayekabiliwa na kesi ya ulanguzi wa madawa ya kulevya.
Alizungumza na Ruth kwanza.