Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Utata kuhusu marufuku ya mikutano ya kisiasa Tanzania
Kumekuwa na maoni tofauti nchini Tanzania baada ya Polisi Nchini humo kupiga marufuku mikutano yote ya ndani ya kisiasa katika hatua ambayo wadadisi wanasema ni jaribio la kukandamiza demkrasia.
Tangazo hilo linafuatia mauaji ya maafisa wanne wa polisi siku ya jumanne katika mji mkuu wa Dar es Salam, mauaji ambayo Polisi inadai yalichochewa kisiasa.
Tayari maandamano na mikutano yote ya hadhara ya kisiasa imeshapigwa marufuku na polisi nchini Tanzania.
"Chama kikuu cha upinzani CHADEMA, kimeshutumu hatua hiyo."
Kutoka Dar es Salaam Mwandishi wetu Ester Namuhisa ametuandalia taarifa ifuatayo.