Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanasiasa Kenya wanawajali vijana?
Nchini Kenya vyama vya kisiasa viko mbioni kwa mipangilio ya kushinda uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.
Ikiwa imesalia chini ya mwaka mmoja kabla ya kura kupigwa, mirengo mipya ya kisiasa imechipuka, vyama vipya vya kisiasa vimetangazwa na mazungumzo ya miungano inaendelea.
Hata hivyo swali linaloonekana kutotiliwa maanani ni je, Vyama vya kisiasa, vinajali maslahi ya vijana?
Ndiyo mada kuu ambayo vijana wanaangazia kuhusu mchango wao katika vyama vya kisiasa.