Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Korir: Wanariadha wa Kenya Olimpiki Rio ni wasafi
Nahodha wa timu ya Kenya, Wesley Korir, amesema wanariadha wote wa Kenya walioko Rio de Janeiro kwa michezo ya Olimpiki hawajatumia dawa za kuongeza nguvu baada ya wote kupimwa na kupatikana bila hatia.
Kwa miaka ya hivi karibuni baadhi ya wanariadha wa Kenya wamefungiwa kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu.
John Nene amezungumza na Wesley Korir mjini Eldoret eneo la Bonde la Ufa.