Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Baiskeli zatumiwa kama ‘daladala’ Shinyanga, Tanzania
Baiskeli hutumika kama chombo cha usafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine, hali ni tofauti mkoani Shinyanga, kaskazini magharibi mwa Tanzania, ambapo baiskeli zinajulikana kama daladala, kutokana na kutumika kibiashara kwa kufanya kazi ya kusafirisha abiria.
Mwandishi wa BBC Esther Namuhisa alizuru Shinyanga hivi karibuni na kutumia usafiri huo wa kipekee daladala.