Muswada wa kutolewa uhai wapitishwa nchini Australia
Eneo la Magharibi mwa Australia limehalalisha kifo kwa hiari kwa wagonjwa mahututi na wale wanaougua magonjwa yasiyo na tiba na limekuwa jimbo la pili katika nchi hiyo kuhalalisha jambo hilo. Mwezi wa Agosti mwanamke mmoja aliyekuwa na saratani alikuwa mtu wa kwanza kumaliza maisha yake chini ya sheria hiyo.
Maoni yako ni yapi kuhusu sheria hii? Tueleze kwenye ukurasa wa Facebook, BBCSwahili.
