Tetesi za Soka Jumamosi: Arsenal wanamtaka Rogers wa Villa

Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal wanamtaka Morgan Rogers, Mohamed Salah anatarajiwa kujiunga na Besiktas, huku Manchester United wakivutiwa na Neco Williams.
Arsenal wamemfanya kiungo mshambuliaji wa Aston Villa na timu ya taifa ya England mwenye umri wa miaka 23, Morgan Rogers, kuwa mlengwa wao mkuu ili kuimarisha safu ya ushambuliaji na wanatarajiwa kuwasilisha ofa, lakini anaweza kugharimu zaidi ya pauni milioni 100. (Sky Sports)

Chanzo cha picha, Getty Images
Gwiji wa Liverpool Mohamed Salah ataendelea na soka yake Uturuki, huku mshambuliaji huyo wa Misri mwenye umri wa miaka 34 akitarajiwa kusajiliwa na Besiktas. (Foot Mercato - in French)

Chanzo cha picha, AFP via Getty Images
Manchester United wanamfuatilia beki wa pembeni wa Nottingham Forest, Neco Williams, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Wales mwenye umri wa miaka 25 akiwa na uwezo wa kucheza pande zote mbili za uwanja. (Football Insider)

Chanzo cha picha, Getty Images
Real Madrid wanamwania winga wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ufaransa, Michael Olise, mwenye umri wa miaka 24, ambaye anashawishiwa na kuhamia Bernabeu. (L'Equipe - in French)

Chanzo cha picha, Getty Images
Tottenham wamekataa ofa ya pauni milioni 46 kutoka Newcastle United kwa ajili ya kiungo wa Sweden mwenye umri wa miaka 20, Lucas Bergvall. (Athletic - requires subscription)
Chelsea watalazimika kulipa pauni milioni 55 iwapo wanataka kumsajili beki wa Crystal Palace na timu ya taifa ya Ufaransa, Maxence Lacroix, mwenye umri wa miaka 26, katika dirisha hili la usajili la majira ya kiangazi. (Times - requires subscription)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa kati wa Celta Vigo na Guinea Ilaix Moriba, 23, amepewa ofa kwa Sunderland, Crystal Palace, Nottingham Forest, Aston Villa na Hull. Anaweza kupatikana kwa takriban euro 20m (£17m). (Nos Diario - in Galician)
Bayern Munich imempa muda zaidi kiungo wa kati wa Ureno Joao Palhinha, 31, ambaye hayupo tena katika mipango ya kocha Vincent Kompany hadi atakaporejea klabuni hapo. Aston Villa wanavutiwa naye. (Record via SportWitness)

Chanzo cha picha, Getty Images
Tottenham wanataka kumsajili winga wa Uholanzi Crysencio Summerville kutoka West Ham. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 huenda akapatikana baada ya The Hammers kushushwa daraja. (Give Me Sport)
Usajili wa wengi uliofanywa na Spurs katika dirisha hili la majira ya kiangazi unamaanisha baadhi ya wachezaji watalazimika kuondoka, huku beki wa Argentina mwenye umri wa miaka 28, Cristian Romero, akitarajiwa kuondoka. (TeamTalk)

Chanzo cha picha, Getty Images
Juventus wameipa Aston Villa ofa ya euro milioni 6.5 (pauni milioni 5.5) kwa ajili ya mlinda lango wa Argentina mwenye umri wa miaka 33, Emiliano Martinez, lakini Villa wanataka euro milioni 12 (pauni milioni 10.2). (La Gazzetta dello Sport - in Italian)

Chanzo cha picha, Getty Images
Juventus wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumnunua mshambuliaji wa Monaco na Marekani Folarin Balogun, 25, huku Borussia Dortmund na Sunderland pia zikimvizia. (Mundo Deportivo - in Spanish)
Manchester United na Newcastle United wanavutiwa na kiungo wa Eintracht Frankfurt na timu ya taifa ya Sweden, Hugo Larsson, mwenye umri wa miaka 22, lakini hakuna klabu yoyote kati ya hizo ambayo bado imewasilisha ofa. (Bild - in German)















