Vita vya Ukraine:Tishio la Urusi laongezeka,wanajeshi wa mstari wa mbele wajawa hofu

Mapigano makali yanaendelea katika eneo la Donbas mashariki mwa Ukraine, huku kukiwa na baridi kali

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Mapigano makali yanaendelea katika eneo la Donbas mashariki mwa Ukraine, huku kukiwa na baridi kali

Wanajeshi wa Ukraine waliokuwa mstari wa mbele katika eneo la Donbas wameiambia BBC kwamba vikosi vya Urusi "vinajifunza kila siku na kubadilisha mkakati wao" huku wakiendelea kupata ushindi katika mji unaozozaniwa vikali wa Bakhmut.

Lakini wanajeshi pia walisisitiza kuwa ari bado iko juu, licha ya kulemewa na uchovu baada ya karibu mwaka mzima wa vita.

Wanajeshi hao wawili wa Kiukreni waliingia ndani ya chumba hicho, wakiwa bado wamejawa na hamaki, wakiwa wametoka tu moja kwa moja vitani kando ya vilima vilivyofunikwa na theluji maeneo ya kusini ya mbali.

Wakiangalia juu ya ramani kubwa kwenye makao makuu ya muda ya kikosi chao, wanabaini kuwa walishambulia mahali ambapo vikosi vya Urusi vilikuwa vikisonga mbele kuelekea kwenye barabara muhimu.

"Ndege ndio mbaya zaidi. Huwezi kuzisikia ukishtukia imetua. Ni sawa na mizinga. Mizinga ni rahisi - angalau unaweza kuwa na sekunde moja au mbili [kupiga mbizi ili kujificha] baada ya kuzisikia zikija, "alisema Sgt Kalchuk.

Kutathmini hali ya jumla ya mzozo kote Donbas ni ngumu sana. Ufikiaji ni changamoto na hatari, na makumi ya vikosi na vikosi tofauti vya Kiukreni vinafanya kazi tofauti, huku kukiwa na usiri fulani, wameenea kwenye mamia ya maili ya mistari ya mbele inayobadilika haraka.

Vikosi vya Ukraine vilifyatua kombora katika Donbas

Chanzo cha picha, Getty Images

Lakini baada ya wiki kadhaa kusafiri katika eneo lote, na kufanya makumi ya mahojiano ya hadharani na majadiliano mapana na wanajeshi wa Ukraine faraghani, nimeshuhudia mada mbalimbali zikiibuka.

Hauhitaji Whatsapp
BBC Swahili sasa kwenye WhatsApp

Pata habari za kina kutoka BBC News Swahili, moja kwa moja kupitia WhatsApp.

Bonyeza hapa kujiunga

Mwisho wa Whatsapp

Kwa muda wa wiki kadhaa, kundi la mamluki nchini Urusi la Wagner limeongoza mapigano mengi karibu na Bakhmut, na kuendeleza idadi kubwa ya wahasiriwa kwa kuanzisha mashambulizi ya karibu ya kujitoa mhanga kwa askari wa miguu katika miji midogo kama Soledar.

Lakini katika siku za hivi karibuni, kulingana na baadhi ya askari wa Ukraine, jeshi la kawaida la Urusi limeanza tena jukumu maarufu, na athari inayoonekana.

"Ni vigumu sana kwetu sasa. Tunaelewa kwamba Urusi inajifunza kila siku na kubadilisha mkakati wao. Na nadhani tunahitaji kujifunza haraka," alisema Dmytro Podvorchanskyi, ambaye anaongoza kitengo cha upelelezi huko Dnipro-1.

Yeye na wengine walizungumza juu ya jinsi vikosi vya kawaida vya Urusi vilivyo na vifaa vya kutosha sasa vilikuwa vikijificha na kusafirisha silaha zao kwa njia bora zaidi na kushambulia njia za usafirishaji wa silaha za Ukraine kwa ufanisi zaidi.

Kutokana na hilo, wanaendelea kupata msingi karibu na Bakhmut na kutishia mji mwingine unaoweza kuwa muhimu, Vuhledar, kusini ya mbali.

uKRAINE

Chanzo cha picha, Getty Images

Lakini bado hakuna dalili kwamba vikosi vya Urusi viko tayari kufanya mafanikio makubwa ya kimkakati. Kamanda mmoja mkuu alisema vifaa vya Magharibi sasa vimeleta usawa kwa kile ambacho kimekuwa vita vya usanifu visivyo na usawa, na kwamba vifaru vya Magharibi hivi karibuni vinaweza kutoa usawa wa jumla kwa upande wa Ukraine.

Ingawa haishangazi kwamba wanajeshi wengi wa Kiukreni wanakabiliwa na uchovu baada ya miezi kadhaa ya migogoro, ari, kwa ujumla, inaonekana kujitahidi.

"Kumekuwa na visa vya askari [wa Kiukreni] ambao hawaonekani kuwa tayari kupigana, na kutofautiana [kuhusu mbinu]," mwanajeshi mmoja wa Ukraine alikiri, akizungumza faraghani.

Wengine walizungumza juu ya kiwewe cha kuona marafiki zao wakifa, vitengo ambavyo vilikuwa na idadi kubwa ya wahasiriwa na athari ya kisaikolojia na mapigano kati kati ya maiti za wanajeshi wa Urusi ambao haiwakukusanywa.

Askari mmoja, akielezea hofu ya uhamasishaji mpya wa Kirusi na ukubwa mkubwa wa usajili wa wapiganaji, alizungumza juu ya hofu yake kwamba "Urusi itatupiga chini".

Lakini baadhi ya askari tuliokutana nao walipuuza mashaka hayo, wakiwalaumu kwa uchovu na - kwa ujumla - kuwasifu makamanda wao kwa kuwapa muda wa kupumzika.

Urusi imeharibu eneo la Donbas kwa mabomu na makombora

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Urusi imeharibu eneo la Donbas kwa mabomu na makombora

Kisingizio kimoja kinachozidi kutolewa kwa mapambano ya Ukraine karibu na Bakhmut ni nadharia kwamba vitengo dhaifu na visivyo na uzoefu sasa vinaachwa kushikilia mstari wa mbele hapa, wakati vikosi vikali vya jeshi vinahamishwa mahali pengine kabla ya shambulio la Ukraine linalotarajiwa, au mashambulio ya kinzani.

Mahali pa mashambulizi yoyote kama haya yanabakia kuwa mada ya uvumi mwingi miongoni mwa askari wa Ukaine.

Wengine wanatarajia msukumo zaidi kaskazini, katika mkoa wa Luhansk, wakati wengine wanashangaa juu ya shambulio la kusini kuelekea Melitopol, ili kutenga na kutishia vikosi vya Urusi ndani na karibu na rasi ya Crimea.

Afisa mmoja mzoefu alisema aliamini kuwa Urusi ilikuwa ikitafuta kunyoosha mstari wake wa mbele, kuchukua sehemu chache zaidi za Donba, na kisha kutangaza "oparesheni imekamilika" na kushinikiza mazungumzo ya amani.

Alisema ana uhakika Ukraine haitakubali kamwe hilo lakini akaonya kwamba jeshi litahitaji ndege za kivita za Magharibi kuvunja ngome zote mpya za Urusi, haswa kusini mwa nchi hiyo.