Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Gharama za vyakula zinavyosababisha ugumu wa maisha Kenya
Zikiwa zimesalia wiki kadhaa kuelekea uchaguzi mkuu nchini Kenya, baadhi ya wananchi wa taifa hilo lenye uchumi mkubwa katika eneo la Afrika Mashariki wanaendelea kulalamikia ugumu wa maisha utokanao na kupanda kwa gharama za bidhaa muhimu kama vile unga, mafuta na bidhaa nyengine.
Hata hivyo, baadhi wana matumaini kwamba, huenda afueni ikapatikana baada ya uchaguzi uliopangwa kufanyika tarehe 9 mwezi wa nane mwaka huu.