Lucius Kawogo: Nilipofuga mende jamii iliniona kichaa,sasa naingiza zaidi ya milioni nane

Lucius ni fundi seremala aliyeamua kugeukia ufugaji wa mende huku akiamini ndio unaompa mafanikio aliyonayo kwa sasa ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba nzuri na ya kisasa pamoja na kuboresha hali yake ya Maisha.

Je mende wana faida gani mwilini? mtu wa lishe toka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ameziainisha faida lukuki kwa walaji wa mende

Je ungependa au utaweza kula mende? kunywa maziwa ya mende je?

Hayo na mengine mengi ungana mwandishi wa BBC Frankmavura aliyefunga safari mpaka Njombe nyumbani kwa Lucius kujionea ufugaji wa wadudu hawa ambao wengi tumezoea kuwaona maeneo ya mazingira machafu.