Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mgogoro wa ugaidi Msumbiji: Watu wanaotekeleza vitendo vya kigaidi ni nani, wanataka nini Msumbiji?
Utekaji nyara, kukata vichwa, na kuchoma nyumba viimekuwa vitendo vya kundi la siri na la kinyama la waasi huko Cabo Delgado, Kaskazini mwa Msumbiji.
Tangu 2017, wamefanya mamia ya uvamizi, na kusababisha idadi isiyojulikana ya vifo na kulazimisha zaidi ya watu 700,000 kukimbia kuyanusuru maisha yao.
Sababu halisi za uasi hazijulikani. Je! Wanaume hawa ni akina nani na wanataka nini?
Kwa kufuatilia harakati za waasi eneoo hilo na mtandaoni, Africa Eye inachunguza kwanini Msumbiji imekuwa eneo maarufu zaidi linalokumbwa na ugaidi kusini mwa Afrika.