Mike brown: Mtanzania anayejizolea maelfu ya dola kwa kufuga mbwa

Kwa miaka sita sasa kijana wa kitanzania Mike brown ana tengeneza zaidi ya shilingi milioni mia moja fedha za kitanzania sawa nawastani wa dolla elfu 45 za Kimarekani kila mwaka kwa kuuza mbwa

Kijana huyu ambaye ana elimu ya shule ya msingi alikuwa mjasiriamali kwa muda akiuza vyombo minadani kabla ya kuhamia kwenye biashara ya simu na sasa mfugaji wa mbwa na mkulima

Mike anaamini iwapo vijana watatumia elimu zao kujiajiri tatizo la ajira litakoma nchini.

Eagan Salla alimtembelea jijini Arusha na hii ni simulizi yake.