Kwanini timu ya Ghana haitamsahau Luis Suarez?

Siku ya Alhamisi, ilikua ni miaka 10 tangu Ghana ilivyopoteza ushindi katika mchuano wa robo fainali dhidi ya Uruguay- kwasababu ya goli la Suarez lenye utata lililofungwa kwa mkono.

Kama Black Stars wangeshinda, wangekua ni timu ya kwanza ya Afrika kufika mbali katika shindano hilo maarufu.

Badala yake bado wanaendelea kuishi na kumbukumbu ya hisia za huzuni ya hali ya juu.