TUAMBIE SIMULIZI YAKO: Je, maisha yako yameathiriwa vipi na kupanda kwa bei ya vyakula?

Familia kote ulimwenguni zinapambana na hali ya kupanda kwa gharama za maisha na watu milioni 71 katika nchi zinazoendelea wanaangukia katika umaskini kutokana na kupanda kwa bei, kwa mujibu wa UN.

Bei za vyakula na uhaba wa chakula vinalazimisha familia kutokula milo mitatu, kutumia viungo vya chakula vya bei rahisi na kuzorotesha afya zao za kimwili na kiakili.

Je, wewe au familia yako mmeathiriwa moja kwa moja na kupanda kwa gharama za chakula? Tuambie jinsi maisha yako yalivyobadilika - ikiwa simulizi yako itachaguliwa, mmoja wa wanahabari wetu anaweza kuwasiliana nawe hivi karibuni.

Tuma swali lako

Our data policy

Ingawa tunalenga kusoma barua pepe zote, hatuwezi kukuhakikishia jibu. Tunaweza kujibu barua pepe yako au kuwasiliana nawe kwa ufafanuzi. Ikifaa, maoni unayotoa yanaweza kuhaririwa na kuchapishwa kwenye vyombo vya habari vya BBC duniani kote. Tafadhali sema katika barua pepe yako ikiwa hutaki maoni yako yachapishwe. Maelezo yako hayatapewa mtu yeyote nje ya BBC bila idhini yako.

BBC ndiyo mdhibiti data ya kibinafsi uliyotoa hapo juu. BBC huchakata data hii kwa misingi ya maslahi yake halali kama shirika la habari ili kuweka rekodi za kihariri. Ikiwa una maswali kuhusu jinsi BBC inavyoshughulikia data yako ya kibinafsi, tafadhali tazama Sera ya Faragha ya BBC: http://www.bbc.co.uk/usingthebbc/privacy/

BBC itahifadhi data yako hadi isiwe na haja tena ya kutathmini na/au kurekebisha masuala yaliyoibuliwa.