Meli ya mafuta yawaka moto kufuatia shambulio la kombora la Houthi

Meli ya mafuta inawaka moto katika Ghuba ya Aden, mwendeshaji wake anasema, baada ya wapiganaji wa Houthis kusema waliishambulia kwa kombora.

Moja kwa moja

  1. Mauaji ya wanawake Kenya: Mamia waandamana kupinga ukatili dhidi ya wanawake

    .

    Chanzo cha picha, Mercy Juma BBC

    Maelezo ya picha, "Niko hapa kwa sababu nina hasira," anasema Winnie Chelagat

    Maandamano yanafanyika katika miji mikuu nchini Kenya kupinga ongezeko la visa vya mauaji ya wanawake na unyanyasaji mwingine dhidi ya wanawake.

    Mamia wamekusanyika Nairobi, Nakuru, Mombasa, Nyeri na Lodwar, wengine wakiwa wamebeba mabango yenye majina ya waliouawa.Utafiti wa 2022 uligundua angalau mwanamke mmoja kati ya watatu wa Kenya alivumilia unyanyasaji wa kimwili wakati fulani maishani mwao."

    Niko hapa kwa sababu nina hasira," Winnie Chelagat mwenye umri wa miaka 33 aliambia BBC."Ni makosa, tumechoka na tunataka kitu kifanyike kuhusu hilo.

    "Wanaume na wavulana lazima wawajibike kwa matendo yao wenyewe badala ya mzigo kuwa kwa wanawake na wasichana kujilinda, alisema mwandamanaji mwingine anayeitwa Michael Onyango.

    "Tunapaswa kuwaelimisha watoto wetu wa kiume na kuwaambia kwamba wanahitaji kuacha kuua wanawake.

    "Maandamano ya Jumamosi yanafuatia mfululizo wa mauaji ya kutisha ya wanawake - ikiwa ni pamoja na mwathiriwa mmoja, ambaye baadaye aliitwa Rita Waeni, ambaye mabaki yake yaliyokatwakatwa yalipatikana yakiwa yameingizwa kwenye mfuko wa plastiki katika nyumba ya kukodisha ya Airbnb.

    Uuaji wa wanawake unafafanuliwa kuwa kuua kwa makusudi mwanamke au msichana kwa sababu wao ni wa kike.

    Shirika la Amnesty International linasema zaidi ya visa 500 vya mauaji ya wanawake vilirekodiwa nchini Kenya kati ya mwaka wa 2016 na 2023.

    Wengi wa wahasiriwa waliuawa na washirika wa karibu au watu wanaojulikana.

    Wanaharakati wanataka mamlaka kuharakisha haki kwa waathiriwa wote wa hivi majuzi wa unyanyasaji wa kingono na kijinsia.

    Makumi ya makundi ya haki za mitaa yanasema kuwa serikali lazima itangaze mauaji ya wanawake kuwa dharula ya kitaifa na mauaji ya tabaka kama uhalifu mahususi, tofauti na mauaji.

    Jijini Nairobi siku ya Jumamosi, waandamanaji waliimba "Sisi ni watu sio wanyama" kwa Kiswahili - wakimaanisha "sisi ni binadamu si wanyama".

    Wengine walibeba mabango yanayosema "wanaume dhaifu tu ndio wanaoua wanawake" na "kila unapomlaumu mwathiriwa unathibitisha muuaji".

    Kushutumu waathiriwa kumeenea kwenye mitandao ya kijamii, huku watoa maoni katika kile kinachoitwa "manosphere" nchini Kenya wakiwalaumu wanawake waliouawa kwa vifo vyao wenyewe.

    Jumbe nyingi kwenye majukwaa ya mtandaoni huzingatia kile waathiriwa walikuwa wamevaa waliposhambuliwa, au huhoji kwa nini hawakutumia simu zao za rununu kuwaambia familia na marafiki waliko.

    Licha ya Kenya kuwa na sheria thabiti dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia, wahalifu wengi hawaadhibiwi.

    Mashtaka yanapoletwa, mara nyingi husonga mbele kwa miaka mingi mahakamani.

  2. Habari za hivi punde, Ving'ora vya onyo la shambulizi la Hezbollah vyalia Israel

    Ving'ora vilisikika katika miji kadhaa ya Israel karibu na mpaka wa Lebanon, kuonya juu ya uwezekano wa shambulio la ndege isiyo na rubani ya Hezbollah.

    Ghasia zinazoendelea mpakani zinakuja huku kukiwa na juhudi za kidiplomasia zinazolenga kuepusha vita kamili na Hezbollah.

    Israel imeonya kuwa "italazimishwa" kuchukua hatua dhidi ya chama hicho, ambacho kinaungwa mkono na Iran, kwa nguvu ikiwa mazungumzo yatashindwa, na hakuna fursa kwa sasa ya kurejea kwa wakaazi waliohamishwa kutoka mpaka wa kaskazini.

  3. Marekani yaidhinisha mauzo ya ndege za kivita za F-16 kwa Uturuki zenye thamani ya $23bn

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, ndege ya F-16

    Serikali ya Marekani imeidhinisha uuzaji wa $23bn (£18bn) wa ndege mpya 40 za kivita za F-16 kwa Uturuki - hatua ambayo ilikuwa imecheleweshwa kwa muda mrefu - baada ya Ankara kuridhia Uswidi kujiunga na Nato.

    Mpango huo unajumuisha vifaa 79 vya kisasa vya ndege za F-16 za Uturuki.

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ililiambia Bunge kuwa imeidhinisha uuzaji wa wapiganaji wa ndege 40 aina ya F-35 kwa Ugiriki, na zitakazogharimu $8.6bn.

    Uturuki iliidhinisha kujiunga na Nato ya Uswidi baada ya kuchelewa kwa zaidi ya mwaka mmoja na kusababisha mvutano katika muungano huo.

    Ilituma ombi la ndege hizo kwa mara ya kwanza mwaka wa 2021, lakini kuchelewa kwake kuridhia zabuni ya Nato ya Uswidi kulionekana kuwa kikwazo kikubwa.

    Uturuki ilikuwa na wasiwasi juu ya kile ilichokiita uungaji mkono wa Uswidi kwa Wakurdi wanaotaka kujitenga.

    Lakini wabunge wa Uturuki waliridhia ombi la Uswidi wiki hii na Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan akatia saini yake ya mwisho.

    Rais wa Marekani Joe Biden kisha akahimiza kwamba mauzo ya F-16 yaidhinishwe "bila kuchelewa".

    Uvamizi kamili wa Urusi nchini Ukraine mnamo Februari 2022 uliongeza umuhimu wa Uturuki kama ngome ya Nato katika eneo la Bahari Nyeusi.

    "Kuidhinishwa kwangu kwa ombi la Uturuki la kununua ndege za F-16 kumetokana na idhini ya Uturuki ya uanachama wa Nato ya Uswidi," Seneta wa Kidemokrasia Ben Cardin, mwenyekiti wa Kamati ya Seneti ya Mahusiano ya Kigeni, mojawapo ya kamati nne muhimu zinazohitaji kuidhinisha uhamishaji wa silaha.

    "Lakini usifanye makosa: Huu haukuwa uamuzi ambao ulikuja kwa urahisi."

    Alisema rekodi ya haki za binadamu ya Uturuki inahitaji kuboreshwa, pamoja na kuiwajibisha Urusi kwa uvamizi wake kamili wa Ukraine.

    Sasa Hungary ndiyo mwanachama pekee wa Nato ambaye bado hajaidhinisha kujiunga kwa Uswidi, ingawa hivi karibuni kumekuwa na dalili kama hizo .

    Mwaka jana, Marekani iliidhinisha kuhamishiwa Ukraine kwa ndege za kivita za F-16 zilizotengenezwa Marekani kutoka Denmark na Uholanzi, mara marubani wa Ukraine walipopata mafunzo kamili ya kuziendesha.

  4. Meli ya mafuta yawaka moto baada ya shambulio la kombora la Houthi

    .

    Chanzo cha picha, Frank Findler

    Meli ya mafuta inawaka moto katika Ghuba ya Aden, mwendeshaji wake anasema, baada ya wapiganaji wa Houthis kusema waliishambulia kwa kombora.

    Kundi hilo la Yemeni lilisema lililenga meli hiyo kwa jina Marlin Luanda siku ya Ijumaa jioni.

    Opereta Trafigura aliambia BBC kwamba mashambulizi yalisababisha moto katika tangi moja la mizigo la meli hiyo na vifaa vya kuzima moto vilikuwa vikitumiwa kuuzuia.

    Jeshi la Marekani lilisema kuwa Wahouthi waliipiga meli hiyo kwa kombora la balestiki .

    Hakuna majeruhi walioripotiwa, Kamanda Mkuu wa Marekani alisema katika taarifa.

    Ni shambulio la hivi punde zaidi dhidi ya meli za kibiashara na Wahouthi wanaoungwa mkono na Iran ndani na karibu na Bahari ya shamu.

    Kundi hilo linasema kuwa linalenga meli katika eneo hilo kuwaunga mkono Wapalestina huko Gaza, ambako Israel inapambana na Hamas.

    Marekani na Uingereza zimeanzisha mashambulizi ya angani dhidi ya wahouthi kujibu, Katika taarifa yake, msemaji wa Houthi alidai kuwa Marlin Luanda ilikuwa meli ya Uingereza na ililengwa kujibu "uchokozi wa Marekani na Uingereza dhidi ya nchi yetu".

    Meli hiyo ya mafuta inapepea chini ya bendera ya Visiwa vya Marshall na inaendeshwa na Trafigura - kampuni ya biashara yenye kampuni katika maeneo 50 duniani kote ikiwa ni pamoja na London.

    Serikali ya Uingereza ilisema mashambulizi dhidi ya meli za kibiashara "hayakubaliki kabisa" na kwamba Uingereza na washirika wake "wanahifadhi haki ya kujibu ipasavyo".

  5. Natumai hujambo