Ushindi wowote wa Zanu-PF nchini Zimbabwe utakuwa wa uongo - Chamisa

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe Nelson Chamisa amesisitiza kuwa ushindi wowote wa chama tawala cha Zanu-PF katika uchaguzi mkuu wa wiki hii hautakuwa dhihirisho sahihi la nia ya wananchi.
Aliiambia BBC kwamba matokeo kama hayo katika kura za urais na wabunge siku ya Jumatano hayatadhihirisha matakwa ya watu, na anadaiwa tayari umeingiliwa na chama tawala na unyanyasaji wa polisi.
Si Zanu-PF wala polisi wamejibu madai hayo. Bw Chamisa, ambaye anaongoza Chama cha Citizens Coalition for Change (CCC), pia aliiambia BBC mamlaka yaliyokuwa yakishikiliwa na Zanu-PF tangu 1980 yanakaribia mwisho, na kwamba ni serikali mpya pekee inayoweza kufufua nchi hiyo.
Zimbabwe iko tayari kwa mabadiliko, Zimbabwe iko huru mwishowe na Zimbabwe itaona uongozi mpya na siasa mpya, siasa mpya zinaanza.
''Sina shaka akilini mwangu kwamba watu wa Zimbabwe wamesema na wameamua kwamba wanataka maisha mapya, na kuna maafikiano kamili kote, kutoka maeneo ya vijijini hadi mijini, ambayo wanahitaji. mabadiliko''.
''Sina shaka katika akili yangu kwamba watu wa Zimbabwe wamesema na wameamua kwamba wanataka maisha mapya, na kuna makubaliano kamili, kutoka vijijini hadi mijini, kwamba wanahitaji mabadiliko''.
''Na sisi ni uso wa mabadiliko, uso wa matumaini, uso wa siku zijazo." kutoka kwa Kiongozi Nelson Chamisa, Chama cha Wananchi (CCC) Na sisi ni uso wa mabadiliko, uso wa matumaini, uso wa siku zijazo."



















