Wizara ya ulinzi ya Urusi: Urusi iko tayari kuzidungua setilaiti za kibinafsi zinazoisaidia Ukraine

Urusi haijaamua kuhusu uwezekano sawa kushambulia setilaiti za kibinafsi za Marekani na nchi nyingine za Magharibi iwapo zitatumiwa kuisaidia Ukraine katika mzozo wa kijeshi.

Moja kwa moja

Dinah Gahamanyi

  1. Mtoto wa Museveni aapa kuwa atakuwa rais Uganda

    Mtoto wa Rais wa muda mrefu wa Uganda Yoweri Museveni kwa mara nyingine tena amezua tetesi kuwa yuko katika mstari wa kumrithi baba yake.

    Jenerali Muhoozi Kainerugaba ameandika kwenye ukurasa wake wa twitter kwamba "atalipa fadhila kwa nchi yake" kwa kuwa rais.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Bw Museveni amekuwa mamlakani tangu 1986 na kuna tetesi za mara kwa mara kwamba Jenerali Kainerugaba anaandaliwa kumfuata.

    Mnamo Mei mwaka huu, mwanajeshi huyo aliuliza kwenye Twitter ikiwa watu walidhani anafaa kugombea urais na mapema mwezi huu aliandika: "Kwa upinzani wa Uganda, baada ya baba yangu, nitawashinda vibaya katika uchaguzi wowote, Waganda wananipenda zaidi kuliko nyinyi''

    Jenerali huyo mwenye umri wa miaka 48 si mgeni kwenye mabishano kwenye Twitter.

    Mwanzoni mwa Oktoba, alitishia katika ujumbe wake wa Twitter kuivamia nchi jirani ya Kenya, na hivyo kusababisha kuomba radhi kwa umma na mikutano ya kidiplomasia ili kuthibitisha uhusiano huo.

    Kisha baadae Rais Museveni kuagiza kwamba akome kutoa maoni yake kuhusu masuala ya serikali kwenye Twitter, Jenerali Kainerugaba alisema kwamba "hakuna mtu atakayempiga marufuku kwa chochote".

  2. Urusi: Ni marufuku na kosa la jinai kutumiana maudhui ya wapenzi wa jinsia moja

    w

    Chanzo cha picha, Reuters

    Urusi inataraji kupitisha muswada wa Marufuku yenye utata dhidi ya kueneza kile kinachoitwa "propaganda za wapenzi wa jinsia moja" inaonekana kuendelezwa kwa watu wazima wote. Hatua hiyo inawakilisha ugumu wa sheria iliyopo ya 2013, ambayo inafanya kutoa taarifa kuhusu wapenzi wa jinsia moja kwa watoto kuwa kosa la jinai.

    Wale waliopatikana na hatia wanakabiliwa na faini kubwa kwa kuendeleza kile Urusi inachokiita "mahusiano ya kingono yasiyo ya kitamaduni".

    Uidhinishaji wa awali wa upanuzi huo ulipigiwa kura na Jimbo la Urusi Duma kwa kauli moja. Mapema wiki hii, maafisa walikuwa wamewataka wanasiasa katika bunge la chini la Urusi kupitisha muda huo - wakionyesha kama sehemu ya vita vya juu zaidi vya maadili ya ustaarabu na Magharibi na kuhusisha na uamuzi wa kuivamia Ukraine.

    Chini ya pendekezo hilo, maelezo kuhusu "mifumo ya maisha yasiyo ya kitamaduni" au "kukataliwa kwa maadili ya familia" yatazingatiwa kisheria kama ponografia, kukuza vurugu, au kuchochea mivutano ya rangi, kikabila na kidini.

    Sheria hiyo pia inakataza maudhui ya watu waliobadili jinsia ambayo huenda "yakasababisha watoto kutamani kubadilisha jinsia zao". Iwapo itapitishwa, sheria itaruhusu taarifa yoyote kwenye mtandao inayojadili mada za LGBT kuzuiwa na filamu zinazochukuliwa kuwa na maonyesho chanya ya kuwa wapenzi wa jinsia moja kupigwa marufuku.

    Wanaharakati wa haki za binadamu na makundi ya LGBT wanasema kurefushwa kwa muda kunamaanisha kuwa kitendo chochote au kutajwa hadharani kwa wapenzi wa jinsia moja ni kosa la jinai.

    Marufuku hiyo pana pia inahusu utangazaji na vitabu - visivyo vya uwongo na fasihi - kuibua wasiwasi wa udhibiti kutoka kwa wachapishaji, ambao wameonya juu ya hatari ambayo inaweza kuathiri vitabu vya zamani vya fasihi ya Kirusi.

    Sheria hiyo inaweka faini ya kati ya rubles 50,000 (£705; $815) na rubles 400,000, huku wasio Warusi wanaokiuka marufuku hiyo wakikabiliwa na kufukuzwa nchini.

    Mswada huo una uungwaji mkono mkubwa lakini kwanza utaidhinishwa na baraza la juu la bunge la Urusi, Baraza la Shirikisho, kabla ya kuidhinishwa na Rais Vladimir Putin.

    Katika hotuba yake iliyojumuisha maeneo manne ya Ukraine mwezi uliopita, Bw Putin alikashifu kuhusu familia zenye "mzazi nambari moja na mzazi nambari mbili" - katika kile ambacho kimefasiriwa kama ukosoaji wa familia za jinsia moja.

  3. Kiongozi wa Burkina Faso hatoajiri mamluki wa Urusi - Marekani

    w

    Chanzo cha picha, Reuters

    Kiongozi wa jeshi la Burkina Faso Ibrahim Traoré amewahakikishia wanadiplomasia wa Marekani kuwa hatawaajiri mamluki wa Urusi kupambana na wapiganaji wa Kiislamu nchini humo, kwa mujibu wa afisa mkuu wa Marekani ambaye amerejea kutoka Afrika Magharibi.

    "Hakuwa na shaka kwa kusema kwamba Burkinabe pekee ndiyo itatetea nchi yao. Hawana nia ya kuwaalika Wagner," Waziri Mdogo wa Masuala ya Kisiasa wa Marekani Victoria Nuland alisema.

    Mataifa ya Magharibi yamelaani nchi jirani ya Mali kwa kupeleka mamluki wa Urusi kupambana na makundi ya kijihadi nchini humo.

    Wanaishutumu Urusi kwa kutoa msaada wa nyenzo katika kutumwa kwa mamluki kutoka kundi la Wagner, ingawa Kremlin inakanusha uhusiano wowote wa serikali na kampuni ya kijeshi ya kibinafsi.

  4. Mwanaume apigwa risasi mbele ya ubalozi wa Urusi nchini Zimbabwe

    Mlinzi wa usalama amempiga risasi na kumjeruhi mwanaume mmoja ambaye alikuwa amavaa sare ya kijeshi nje ya ubalozi wa Urusi katika mji mkuu Harare Jumatano usiku, polisi imesema.

    Msemaji wa polisi Paul Nyathi ameiambia BBC kuwa mwanaume huyo mwenye umri wa miaka 24 alikuwa amekabiliana na walinzi wa usalama katika ubalozi huo.

    Alipelekwa katika hospitali yae neo hilo ambako ameendelea kushikiliwa huku polisi wakiendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo.

    Afisa habari katika ubalozi wa Urusi , Egor Kuropitnik, ameiambia BBC kuwa picha za uchunguzi zilionyesha kuwa mwanaume huyo alikuwa akitembea kuelekea walipokuwa walinzi.

    Wakati alipokaribia ukuta wa ubalozi ofisa alifyatua kile ambachio kingekuwa ni risasi ya tahadhari, lakini mwanaume huyo aliendelea kusonga mbele kuelekea eneo la usalama. Risasi ya pili ilifyatuliwa na mwanaume akaanguka.

    Hakuonekana kwamba alikuwa anajaribu kupanda ukuta wa uzio wa ubalozi, Bw Kuropitnik alisema.

  5. Habari za hivi punde, Wizara ya ulinzi ya Urusi: Urusi iko tayari kuzidungua setilaiti za kibinafsi zinazoisaidia Ukraine

    G

    Chanzo cha picha, SPACEX

    Naibu mkuu wa idara ya - kitengo cha udhibiti wa silaha za nyukliana silaha nyinginezo katika Wizara ya mambo ya nje ya Urusi , Konstantin Vorontsov, amesema Alhaisi kuwa Urusi haijaamua kuhusu uwezekano sawa kushambulia setilaiti za kibinafsi za Marekani nan chi nyingine za Magharibi iwapo zitatumiwa kuisaidia Ukraine katika mzozo wa kijeshi.

    Hili lilitangazwa wakati wa mkutano wa Kamati ya kwanza ya Mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa.

    "Kando ha hayo, tungependa kusisitiziakuhusu shughuli hatari ambazo zimejidhihirisha zenyewe katika vita vya Ukraine.

    Tunazungumzia kuhusu matumizi ya Marekani na washirika wake ya miundo mbinu ya raia iliyopo katika anga za mbali, ikiwemo ya kibinafsi, katika mzozo wa kivita. Miundo mbinu ya kiraia ya Quasi inaweza kugeuka kuwa ya kulengwa na mashambulio halali katika kulipiza kisasi." , - Shirika la habari la Urusi TASS lilimnukuu Vorontsov.

    Nchini Ukraine, mfumo wa mawasiliano ya setilaiti ya wa anga za mbali wa SpaceX unaomilikiwa na tajiri Elon Musk unajukumu kubwa katika mawasiliano nchini humo.

    Kulingana na vyanzo vya habari vya Ukraine, nchi hiyo pia hivi karibunni imeweza kupata mawasiliano kutoka kwenye setilaiti za kampuni ya Finland inayofahamika kama ICEYE.

    Vita vya Ukraine: Mengi zaidi

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
  6. Kenya: Baraza jipya la mawaziri la Rais William Ruto kuapishwa leo

    G

    Chanzo cha picha, EPA

    Baraza jipya la mawaziri 22 nchini Kenya linatarajiwa kuapishwa Alhamisi, siku moja baada ya kuidhibishwa na bunge.

    Rais William Ruto amebakia na waziri mmoja kutoka katika baraza la mawaziri la mtangulizi wake kama mshauri wa masuala ya usalama na kuanzisha wadhifa wa Waziri mkuu.

    Gavana wa zamani wa benki kuu, Njuguna Ndung’u, atakuwa Waziri wa fedha, huku spika wa zamani, Justin Muturi, atakuwa mwanasheria mkuu wa umma.

    Rais aliwazawadia wanasiasa washirika wake kwa kuwateua kuwa mawaziri.

    Ingawa aliahidi kuwa 50% ya mawaziri atakaowateua watakuwa ni wanawake, Bw Ruto aliwateua wanawake saba pekee katika baraza hilo, huku wanawake wawili wakiteuliwa kuwa washauri wa rais na mmoja kama katibu wa baraza la mawaziri.

    Jukumu la moja kwa moja la baraza jipya litakuwa ni kupunguza garama ya maisha na mzozo wa chakula uliosababishwa na ukosefu wa mvua.

    Jumanne, rais alisema kuwa atahitaji walau mwaka mmoja kupunguza bei ya unga wa mahindi – unaotumiwa kupika ugali, ambacho ni chakula kikuu nchini humo.

  7. Mawaziri wa Uganda kuanza mafunzo ya lugha ya Kiswahili

    g

    Chanzo cha picha, Rebecca Kadga/Twitter

    Maelezo ya picha, Naibu wa kwanza wa Waziri mkuu na Waziri wa masuala ya Afrika Mashariki Rebecca Kadaga, anasema mafunzo yatawawezesha mawaziri kuzungumza lugha ya Kiswahili

    Baraza la mawaziri cha Uganda, linalokaa kila Jumatatu na kuongozwa na rais, limeidhinisha kuanza kwa masomo ya lugha ya Kiswahili kwa chache asubuhi kwa mwaka mmoja ujao. Hii ni kwa mujibu wa Naibu wa kwanza wa Waziri mkuu na Waziri wa masuala ya Afrika Mashariki Rebecca Kadaga.

    Kadaga, ambaye alikuwa akifungua mkutano wa mwaka unaoendelea wa Mahakama ya kisheria ya Afrika Kusini mjini Kampala, alisema hii itawawezesha wajumbe kuanza kufanya mikutano kwa Kiswahili.

    Uganda iliidhinisha lugha ya Kiswahili kama lugha ya pili rasmi baada ya Kiingereza na kuagiza shule kuifanya lugha hiyo kuwa ya lazima.

  8. Vita vya Ukraine: Rais wa Israeli asema kuna masharti kuhusu upelekaji wa mifumo ya ulinzi Ukraine

    G

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Rais wa Israeli Yitzhak Herzog amesema kuwa kuna masharti ambayo yanazuia usambazaji wa mifumo fulani ya ulinzi kwa Ukraine. Israeli, alisema iko tayari kuipatia Ukraine silaha zisizo za sumu.

    “ Kuna silaha ambazo hatuwezi kuzisafirisha. Kuna vitu ambavyo havipaswi kufikia mikononi mwa maadui zetu. Kuna siri ambazo hatuwezi kuzitoa. Lakini pale tunapoweza kusaidia, tunajaribu kusaidia ,” alisema katika mahojiano na televisheni ya CNN.

    Herzog hakubaliani na ukosoaji wa msimamo wa Israeli kuhusu kutuma silaha nchini Ukraine, akisema kuwa Marekani na Ulaya zilikuwa zimekataa kuipatia serikali ya Kyiv baadhi ya vifaa vya kijeshi.

    Pia alisema kuwa Israeli inatathmini hali ya Urusi kutumia ndege zisizokuwa na rubani (droni ) zilizotengenezwa na Iran.

    Tangu ilipoanza uvamizi dhidi ya Ukraine, Urusi imetumia droni 400 kutoka Iran kushambulia watu na miundo mbinu, alisema rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky Jumatano.

    Awali alisema kuwa Urusi inaweza kuilipa Iran pesa za droni kwa ajili ya kuusaidia mpango wa nyuklia wa Iran.

    Rais huyo wa Israeli alisema hana taarifa maalum kuhusu mkataba wa aina hiyo, lakini akasemakwamba "hakuna haja ya ushahidi wa ziada kwamba Iran inasababisha tisho la usalama na uthabiti wa dunia."

    Vita vya Ukraine: Mengi zaidi

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
  9. Vita vya Ukraine: Mbinu za Urusi katika maeneo ya vita ya mashariki ni za 'kinyama', asema Zelensky

    G

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Maelezo ya picha, Kifari cha kijeshi cha Ukraine kikielekeakatika Bakhmut

    Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ameiwashutumu makamanda wa Urusi kwa "unyama" katika juhudi zao za kuuteka mji wa mashariki mwa nchi hiyo wa Bakhmut.

    Mji huo – ambao upo katika jimbo la Donetsk na ambao ulikuwa unakaliwa na watu 70,000 kabla ya vita – umekuwa kitovu cha mashambulio ya Urusi kwa miezi kadhaa.

    Licha ya kukaribiwa kwa Waukraine katika mji muhimu wa Kherson, Bw Zelensky alisema mashambulio yanaendelea kwa nguvu.

    Kunyakuliwa kwa mji huo kutakuwa ni alama ya ushindi kwa Urusi.

    "Hapa ndipo unyama wa makamanda wa Urusi unapodhihitika," Alisema Bw Zelensky katika hotuba yake kutoka Kyiv. "Siku baada ya siku,kwa miezi, wanawapeleka watu kufia pale, wakiwapiga kwa mashambulizi ya kiwango cha juu ya makombora."

    Mshauri wa ngazi ya juu wa Bw Zelenskym, Oleksiy Arestovych alisema kuwa kwa siku moja vikosi vya Urusi vilifanya mashambulio manane tofauti katika katika Bakhmut kabla ya muda wa mlo wa mchana na yamekuwa yakisukumwa nyuma kila mara yanaposhambulia.

    Mji huo uko kwenye barabara kuu inayoelekea katika miji inayodhibitiwa na Ukraine ya Sloviansk na Kramatorsk.

    Vita vya Ukraine: Mengi zaidi

    • YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
    • UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
    • UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
    • KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
    • ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
    • PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine
  10. Ujerumani inapanga kuhalalisha bangi kama kiburudisho

    G

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Mwaka huu katika maandamano ya Hemp mjini Berlin: Ujerumani inaweza kuwa nchi inayoongoza Ulaya kwa bangi

    Serikali ya muungano ya Ujerumani imekubaliana juu ya mpango wa kuhalalisha kisheria matumizi ya bangi kama kiburudisho miongoni mwa watu wazima.

    Mtu ataruhusiwa kumiliki na hadi gramu 30 (1oz) kwa ajili ya matumizi ya kibinafsi. Maduka ya kawaida yaliyopewa leseni na maduka ya dawa yatauza bangi.

    Mpango bado haujaidhinishwa katika bunge – lakini umeidhinishwa na Tume ya Muungano wa Ulaya. Waziri wa afya wa Ujerumani Karl Lauterbach alisema kuwa mpango huo unaweza kuwa sheria katika mwaka 2024.

    Katika Muungano wa Ulaya ni Malta pekee ambayo ilihalalisha kisheria matumizi ya bangi kama kiburudisho.

    Uholanzi imefikia hatua sawa na mpango wa Ujerumani - chini ya sheria ya Uholanzi, mauzo ya kiasi kidogo cha bangi "katika maduka ya kuuza kahawa" yanakubalika.

    Mpango wa Ujerumani pia utaruhusu nyumba kupanda mimea mitatu ya bangi kwa kila mtu mzima.

    Hatua hiyo ilikuwa ni miongoni mwa ajenda za serikali ya muungano, zilizotangazwa mwaka jana. Muungano huo unaongozwa na Chama cha Social Democrats (SPD) kikiwa pamoja na kile cha Kijani na liberal Free Democrats kama washirika.

    Nchi kadhaa zimehalalisha kisheria matumizi madogo ya kimatibabu ya bangi. Canada na Uruguay pia zimehalalisha bangi kama kiburudisho.

    Unaweza pia kusoma:

    • Bangi: Zijue nchi tano zilizoruhusu uzalishaji wa bangi Afrika
    • Kwa nini mataifa mengi yameanza kuidhinisha matumizi ya bangi?
  11. Watoto sita wa familia moja wapatikana na Ebola Uganda

    G

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Watoto sita wa familia moja ya Kampala wamepata maambukizi ya ugonjwa wa Ebola, wamesema maafisa katika mji mkuu Kampala.

    Kwa wiki nne madaktari wamekuwa wakitoa wito wa hatua kali za kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya virusi mjini Kampala.

    Virusi vya Ebola vinaweza kusambaa haraka katika maeneo yanayokaliwa na watu wengi na aina hii ya Ebola- inayoitwa Ebola ya Sudan – haina chanjo.

    Mapema mwezi huu wilaya ambazo zimeathirika zaidi na mlipuko, Mubende na Kassanda ziliwekwa katika karantini.

    Watoto hao sita ndugu wa familia moja walipata maambukizi baada ya ndugu yao aliyetoka katika moja ya wilaya zilizoathiriwa zaidi kuja kuishi nao, na baadaye kufariki, wamethibitisha maafisa wa afya.

    Tangu mlipuko ulipoanza Mwezi Septemba, wizara ya afya ya Uganda imerekodi visa 109 na vifo 30. Kufikia Jumatatu, vifo 15 kati ya hivyo vilitokea mjini Kampala.

    Baadhi wanahofia kuwa Rais Yoweri Museveni alichelewa kushughulikia hatua za tahathari za mapema zilizotolewa na wahudumu wa afya kuhusu virusi hivyo vya homa inayosababisha kuvuja kwa damu.

    Waziri wa afya Jane Ruth Aceng anasema anahofu kubwa kuhusu kusambaa kwa virusi katika maeneo ya mijini, ambako kuna idadi kubwa ya watu.

    Watoto hao ndugu sita waliopatikana na Ebola katika mji mkuu hawajatajwa majina yao wala umri wao haujafichuliwa, ili kulinda utambulisho wao.

    Lakini tunafahamu kuwa shule wanakosoma watoto hawa bado haijafungwa.

    Dkt. Aceng anasema wahudumu wa afya sita ambao walipata maambukizi baada ya kuwatibu wagonjwa pia ni miongoni mwa wale waliofariki hivi karibuni.

    Kampala ni mji wa kiuchumi na iwapo Ebola itasambaa haraka mjini humo, kuna hatari kubwa ya virusi hivyo kusambaa katika nchi nyingine.

  12. Hujambo na karibu tene kwa matangazo yetu mubashara leo ikiwa ni Alhamisi tarehe 27.10.2022