Uchunguzi waidhinishwa kubaini chanzo cha ajali

Siku moja baada ya ajali ya ndege ya Ethiopian airlines kuanguka, sasa angazio ni kubaini chanzo cha ajali ya ndege hiyo chapa Boeing 737 Max ambayo ni ya tano ya aina ya ndege hiyo katika miezi mitano - na ikiwa ni ndege mpya.

Moja kwa moja

  1. 'Hatutishwi na uamuzi wa Facebook'

    Waziri wa habari nchini humo Paul Fletcher ameiambia BBC kuwa kampuni hiyo inahitaji kufikiria kwa uangalifu kuhusu hatua walioichukua

    Waziri Mkuu wa Australia Scott Morrison amesema kuwa serikali yake haitishwi na kitendo cha Facebook kuzuia kupatikana kwa habari nchini humo.

    Kampuni ya Facebook imezuia watumiaji wake nchini Australia kuchapisha au kutazama habari katika jukwaaa hilo jambo lililozua wasiwasi mkubwa miongoni mwa watumiaji wa mtandao huo wa kijamii kuhusu namna watakavyopata habari muhimu na kuchangamana pia.

    Wale walio nje ya Australia pia hawawezi kusoma au kupata machapisho yoyote ya habari ya Australia kwenye jukwaa hilo la facebook.

    Aidha kampuni ya facebook imechukua hatua hiyo baada ya kuwepo sheria ambayo nchi hiyo inapanga kuwatoza pesa wafanyabiashara wanaochapisha habari kwenye jukwaa hilo.

    Aidha kampuni kama Google na Facebook wamesema sheria hiyo haielezi wazi jinsi mtandao huo utakavyofanya kazi na hivyo umelenga kuwaadhibu tu.

    Lakini serikali ya Australia imesema kuwa inaendelea na sheria hiyo, ambayo ilipitishwa na baraza la bunge siku ya Jumatano.

    Waziri wa habari nchini humo Paul Fletcher ameiambia BBC kuwa kampuni hiyo inahitaji kufikiria kwa uangalifu kuhusu hatua walioichukua.

  2. Habari! karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya taarifa zetu

  3. Virusi vya corona: Burundi yafungua anga lake kwa Ndege za kimataifa kuingia

    Kuanzia siku ya Jumapili, Uwanja wa ndege wa Bujumbura umefunguliwa kwa ajili ya ndege zinazofanya safari kimataifa baada ya kufungwa kwa miezi saba kutokana na janga la virusi vya corona.

    Burundi imekuwa nchi ya mwisho ya Afrika mashariki kufungua anga yake baada ya Tanzania mwezi May, Sudani Kusini mwezi Julai, Kenya na Rwanda mwezi Agosti na Uganda mwezi Septemba.

    Mamlaka ya anga imesema, abiria watakaoingia watahitajika kuwasilisha cheti kinachoonesha majibu ya vipimo vilivyofanywa saa 72 zilizopita yanayoonesha kutokuwa na maambukizi ya virusi, kufanyiwa vipimo na kukaa karantini kwa saa 72, kwa gharama zao.

    Melance Ndayisenga, mkazi wa jiji la Bujumbura, amefurahishwa na kufunguliwa kwa uwanja wa ndege lakini amesema sekta ya utalii imeporomoka kutokana na kufungwa kwa uwanja huo wa ndege.

    Burundi mpaka sasa imerekodi maambukizi kwa watu 421 na kifo cha mtu mmoja.

  4. Bunge la 12 kuanza leo Tanzania

    Shughuli za bunge kuanza asubuhi hii nchini Tanzania

    Chanzo cha picha, Bunge

    Bunge la 12 linaanza rasmi hii leo huko jijini Dodoma katikati mwa Tanzania.

    Hii leo Spika wa bunge na naibu wake watachaguliwa rasmi na baadae kufuatia shughuli ya wabunge waliochaguliwa kula viapo vya utii.

    Hata hivyo kuna maswali mengi yanaulizwa iwapo bunge hili ambalo asilimia zaidi ya 80 ni kutoka chama tawala cha CCM litaweza kuisimamia vyema serikali katika shughuli zake.

  5. Habari! Karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya taarifa zetu hii leo.

  6. Asante!

    Asante kwa kujumuika nasi kupata taarifa mbalimbali kuhusu taarifa baada ya ajali ya ndege nchini Ethiopia.

  7. Mashirika ya ndege yanayotumia Boeing 737 Max 8 Afrika

    Yapo mashirika manne ya ndege Afrika yaliyo na ndege aina ya Boeing 737 Max 8, ndege sawa na iliyoanguka muda mfupi baada ya kupaa kutoka Addis Ababa, Ethiopia Jumapili.

    Shirika la ndege la Comair kutoka Afrika Kusini lilipokea ndege yake ya kwanza ya aina hiyo wiki mbili tu zilizopita.

    Ndilo shirika la kwanza kusini mwa Afrika kuwa na ndege kama hiyo, na linatarajiwa kupokea ndege nyingine ya Max 8 baadaye mwezi huu, na nyingine sita baadaye

    Comair wametoa taarifa wakisema wataendelea kufuatilia kwa karibu uchunguzi unaofanyika kuhusu ajali hiyo ya ndege ya Ethiopian Airlines na wanawasiliana na Boeing na Shirika la Safari za Ndege la Afrika Kusini.

    Kwa mujibu wa Boeing, shirika la Mauritania Airlines lilikuwa la kwanza kupokea ndege aina ya Boeing 737 Max 8, ndege ambayo waliipokea Desemba 2017.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

    Ethiopian Airlines walipokea ndege yao ya kwanza aina ya Max 8 Julai 2018. Kampuni hiyo ilikuwa imeagiza jumla ya ndege 30 za aina hiyo.

    Shirika hilo la ndege la Ethiopia limesitisha safari za ndege nne za aina hiyo zilizosalia, huku uchunguzi ukiendelea kujaribu kubaini chanzo cha ajali hiyo ya Jumapili.

    Shirika la Royal Air Maroc la Morocco nalo lilipokea ndege ya kwanza ya 737 Max 8 December mwaka jana, na walipokea nyingine Februari mwaka huu.

    Yapo mashirika mengine yanayosubiri kupokea ndege za aina hiyo karibuni.

    Septemba 2018, shirika la Air Peace of Nigeria liliagiza jumla ya ndege 10 kama hizo.

    Miezi mitatu baadaye, Boeing walitangaza kwamba shirika jingine la Nigeria, Green Africa Airways lilikuwa limeeleza ahadi ya kununua ndege 100 kama hizo, linapojiandaa kuanza shughuli.

    Ununuzi wa ndege hizo ulitarajiwa kugharimu $11.7bn (£9bn), na ungekuwa ndio mkataba wa thamani ya juu zaidi wa ununuzi wa ndege kuwahi kutiwa saini kati ya shirika la ndege la Afrika na kampuni ya Boeing.

  8. Indonesia yasitisha safari za Boeing 737 Max-8

    Indonesia imejiunga na Ethiopia na China katika kusitisha safari za ndege aina ya Boeing 737 Max-8 baada ya ajali ya Ethiopian Airlines.

    "Ukaguzi" wa ndege hizo utafanyika, na ni 'marufuku kwa muda' ndege hizo kusafiri, mkurugenzi mkuu wa usafiri wa anga Indonesia, Polana Pramesti, amesema.

    eneo la mkasa

    Chanzo cha picha, Reuters

  9. Mambo muhimu katika ajali ya ndege ya Ethiopia Airlines

    Kuanzia safari ilipoanza mpaka ajali ilipotokea ya ndege ya Ethiopia Airline ET302,

    Maelezo ya video, Ajali ya Ethiopia Airlines ET302
  10. Ndugu wa waliopoteza maisha kusaidia utambuzi Ethiopia

    Waziri wa usafirishaji James Macharia amesema serikali itawasafirisha kuelekea Ethiopia ndugu wa waliopoteza maisha kwa ajali ya Ndege siku ya Jumapili mjini Addis Ababa, ili waweze kusaidia kutambua miili. Akizungumza na waandishi wa habari ,macharia amesema familia 25 kati ya 32 tayari wamepatiwa taarifa na taratibu za kupata familia zilizobaki zinaendelea. Waziri amesema, zoezi la usafirishaji litafanywa kwa ushirikiano na serikali ya Ethiopia na Kenya pia Shirika la ndege la Kenya Airways na Ethiopian airlines. Ethiopian airlines lilitangaza kusafirisha miili kuelekea Kenya baada ya kumaliza shughuli za uthibitisho. Katika hatua nyingine, ndege zote za Ethiopia zinazohusisha Boeing 737 MAX 8 jeti zimesitisha safari zake kwa sababu za kiusalama na uchunguzi kuhusu sababu za ajali ya siku ya Jumapili.

    Familia za watu 25 zimeshatambulishwa ndugu zao

    Chanzo cha picha, JONATHAN DRUION

    Maelezo ya picha, Familia za watu 25 zimeshatambulishwa ndugu zao
  11. Ndege namba ET 302 yatua Nairobi

    Ndege namba 302 kutoka Ethiopian Airlines imetua siku ya Jumatatu katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.Namba ya ndege hiyo ni kama ile iliyopata ajali siku ya Jumapili, dakika sita baada ya kupaa kutoka uwanja wa kimataifa wa Bole mjini Adis Ababa.Mhariri wa habari za biashara,BBC ameandika kwenye ukurasa wake wa Twitter akiwa uwanja wa ndege Nairobi.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe

  12. Habari za hivi punde, Kisanduku cha kunakili data ya safari ya ndege kimepatikana,

    Kisanduku cha kunakili data ya safari ya ndege ya Ethiopian Airlines ET 302 iliyoanguka Jumapili mjini Bishoftu, 60km kusini mashariki mwa mji mkuu, Addis Ababa, kimepatikana, Vyombo vya habari Ethiopia vinaripoti.

    Mwandishi wa BBC anaeleza kwamba duru kutoka kampuni hiyo ya ndege Ethiopian imethibitisha kwamba 'black box' kimepatikana ila kimeharibika kidogo.

    Kampuni ya kutengeneza ndege ya Boeing ilioko Marekani inakabiliwa na maswali baada ya ndege hiyo kuanguka dakika sita baada ya kupaa na kusababisha vifo vya watu 157.

  13. Maafisa kazini

    Wafanyakazi wa kikosi cha uokoaji wakikusanya mabaki ya miili ya abiria waliopoteza maisha kutokana na ajali.

    Maafisa wanasema ni shughuli inayohitaji umakini mkubwa

    Chanzo cha picha, Reuters

    Maelezo ya picha, Maafisa wanasema ni shughuli inayohitaji umakini mkubwa
  14. Yaliobaki katika eneo la mkasa

    Baadhi ya vitu vilivyosalia katika eneo ambako ndege ya Ethiopia Airlines imeanguka.

    eneo la mkasa

    Chanzo cha picha, Reuters

    kiatu cha abiria

    Chanzo cha picha, Reuters

  15. 'Nguo, paspoti, na kompyuta zimetapakaa katika eneo la mkasa'....

    Maafisa wa uchunguzi na vikosi vya uokozi wamekuwa wakipekuwa masalio ya ndege ET 302 tangu Jumapili asubuhi wakati ilipoanguka muda mfupi baada ya kuondoka.

    Ni shughuli ya taratibu na inayohitaji umakini mkubwa anasema mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza aliye katika eneo la mkasa kutokana na kwamba sehemu kubwa ya ndege hiyo imevunjika vipande vipande baada ya kuanguka katika ardhi inayotumika kwa ukulima karibu na mji wa Bishoftu.

    Masalio ya ndege hiyo na, mali binafsi ya abiria waliofariki zimepatapakaa katika sehemu ya mkasa.

    Wachimbaji wamefika kulima katika shimo lililozuka kutokana na athari ya ndege hiyo kuanguka.

    Maafisa wanasema lengo ni kukusanya masalio zaidi ya watu waliofariki katika ajali hiyo.

    Wanatafuta pia kisanduku kinachonakili rekodi za safari ya ndege hiyo, 'black box' kitakacho toa taarifa muhimu zitakazosaidia kupata picha halisi ya nini hasaa kilichotokea kabla ya ndege hiyo ET 302 ilipoanguka.

    Kampuni iliyotengeneza ndege hiyo Boeing imesema wachunguzi wake watajumuika na kikosi kilichopo kutafuta sababu kwanini ndege hiyo imeanguka.

    Waziri mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed ameahidi uchunguzi wa kina kuhusu ajali hiyo na ameahidi kuweka wazi matokeo ya uchunguzi huo.

    wreckage

    Chanzo cha picha, Getty Images

  16. Shughuli ya kukusanya masalio ya ndege,

    Mwandishi wa BBC Emmanuel Igunza yupo katika eneo la mkasa ambapo maafisa kwa sasa wanakusanya masalio ya ndege Boeing 737 Max iliyoanguka Ethiopia

    Maelezo ya video, Boeing 737 Max 8: Maafisa wakusanya masalio ya ndege Ethiopia
  17. Bendera zapepea nusu mlingoti,

    Ethiopia imetangaza siku ya maombolezi , kuwakumbuka waliofariki katika ajali ya ndege na bendera zinapepea nusu mlingoti.

    Bendera zinapepea nusu mlingoti
  18. Ukimya, kuwakumbuka marehemu,

    Wafanyakazi wa tume ya uchumi katika Umoja wa mataifa kwa bara la Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia, wamekusanyika leo kuwakumbuka wafanyakazi wenzao waliofariki katika ajali ya ndege ya Ethiopia Airlines.

    Wafanyakazi wa tume ya uchumi katika Umoja wa mataifa kwa bara la Afrika, wakusanyika kuwakumbuka wafanyakazi wenzao waliofariki katika ajali ya ndege ya Ethiopia Airlines
    Maelezo ya picha, Wafanyakazi wa UN ECA wakusanyika kuwakumbuka wenzao waliofariki katika ajali ya Ethiopia Airlines
  19. Umoja wa mataifa waomboleza maafisa wake

    Katibu mtendaji wa tume ya uchumi katika Umoja wa mataifa kwa bara la Afrika, imeeleza kushtushwa kwake na huzuni kwa mkasa huo wa ndege uliosababisha vifo vya maafisa kadhaa wa mashirika ya Umoja huo wa mataifa, na pia katika mashirika mengine ya kimataifa, imeeleza taarifa ya uneca.

    ”Tunawafikiria na kuziombea familia, marafiki wa karibu na wafanyakazi wenza wa waathiriwa wa mkasa wa ndege” amesema Bi. Songwe.

    Ruka X ujumbe
    Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

    Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

    Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje

    Mwisho wa X ujumbe