Tsvangirai ashangazwa na hatua ya Mugabe

Chanzo cha picha, EPA
Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe Morgan Tsvangirai ambaye wakati mmoja alihudumu kama waziri mkuu katika serikali ya umoja wa taifa na Rais Robert Mugabe ameambia shirika la habari la Reuters kwamba ameshangazwa sana na hotuba ya Mugabe.
Sawa na baadhi ya raia wengine Zimbabwe, kiongozi huyo wa chama cha Movement for Democratic Change (MDC) amesema alikuwa anamtarajia Mugabe, 93, ajiuzulu baada ya jeshi kuchukua udhibiti wa serikali wiki iliyopita.








