Tetesi za Soka Ulaya Jumatano: Liverpool yamfuatilia Thiaw

Chanzo cha picha, Getty Images
Liverpool na Manchester United zinaendelea kumfuatilia beki wa Ujerumani, Malick Thiaw, mwenye umri wa miaka 25, lakini Newcastle haina mpango wa kumuuza. . (Caught Offside)
Winga wa Sunderland, Chemsdine Talbi, mwenye umri wa miaka 21, yuko mbioni kujiunga na klabu ya Al Ittihad ya Ligi Kuu ya Saudi Arabia.
Fulham inatarajiwa kuanza mazungumzo ya kuongeza mkataba wa beki wake, Calvin Bassey, mwenye umri wa miaka 26, anayewindwa na Inter Milan.
Winga wa Bournemouth, Rayan, mwenye umri wa miaka 20, ana kipengele cha kuvunja mkataba chenye thamani ya pauni milioni 130, kitakachoanza kutumika katika dirisha la usajili la majira ya joto 2027. (David Ornstein via the Athletic - subscription required)
Newcastle itampa kiungo Joe Willock, mwenye umri wa miaka 27, mkataba mpya iwapo ataendelea kuonyesha kiwango kizuri chini ya kocha Matthias Jaissle. (Football Insider)
Kiungo wa zamani wa Real Madrid, James Rodriguez, mwenye umri wa miaka 35, yuko kwenye mazungumzo ya kujiunga na Avellino ya Serie B, inayofundishwa na beki wa zamani wa Italia, Alessandro Nesta.(Marca)
Chelsea iko tayari kuwasilisha ofa kwa kiungo wa Bournemouth, Alex Scott, mwenye umri wa miaka 23, katika dirisha la usajili la Januari(Teamtalk)

