Majambazi yavamia kituo cha Redio na kupora matangazo yakiendelea
Maafisa wa upelelezi katika Kaunti ya Nakuru nchini Kenya wanasaka taarifa kuhusu majambazi waliojihami kwa silaha waliovamia kituo cha redio, kuwatapeli wafanyakazi na kuchukua pesa taslimu na vitu vingine vya thamani.
Katika tukio hilo lililorekodiwa moja kwa moja na kamera, majambazi hao waliokuwa na silaha za moto na mapanga walinaswa walipokuwa wakiingia kwenye studio ya Mwinjoyo FM, ambapo waliwaamuru watangazaji walale chini kabla ya kupora fedha na vitu vingine vya thamani.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
“Zima kitu hicho! Lala chini,” mmoja wao aliamuru huku watangazaji wawili mwanamume na mwanamke wakilala chini. Majambazi hao ambao walikuwa wameficha nyuso zao walikatiza matangazo ya moja kwa moja ya kipindi cha injili yaliyokuwa yakiendelea.
Genge hilo la watu wanne liliondoka na simu 8, pesa taslimu zaidi ya Sh35,000 na jozi nane za viatu. Kamera tano pia ziliharibiwa na majambazi hao kabla ya kukimbia kwa kuruka uzio wa eneo hilo lililoko katika vitongoji vya kifahari vya Nakuru Milimani.
Kwa mujibu wa taarifa Msako wa kuwasaka majambazi hao waliovalia nguo nyeusi umeanza.










