Kukulia gerezani: Watoto wanaamini gereza ni nyumbani

Maelezo ya video, Utata juu ya watoto wanaolelewa gerezani kando na mama zao wafungwa

Nchi nyingi kote duniani huwaruhusu watoto kuishi na mama zao waliofungwa gerezani.

Hatahivyo, suala hilo ni tata, huku baadhi ya watu wakidai kuwa gereza sio mazingira mazuri ya malezi kwa mtoto.

Nchini Kenya watoto wapatao 200 kwa sasa wanaishi magereza ambako mama zao wanatumikia kifungo na suala hili limeibua mjadala nchini humo juu ya ni hatua gani zinazofaa kuchukuliwa kuwasaidia watoto hao. Mwandishi wa BBC Agnes Penda ana taarifa zaidi.