Nilimkatisha mwanangu kunyonya ili nimnyonyeshe mtoto wa dadangu aliyefariki dunia

Maelezo ya video, Nilimkatisha mwanangu kunyonya ili nimnyonyeshe mtoto wa dadangu aliyefariki dunia

Asha Aboubakar mkazi wa Ngusero jiji Arusha alilazimika kumkatisha kunyonya mwanae mwenye mwaka mmoja na nusu ili amnyonyeshe mtoto mchanga wa mdogo wake aliyefariki muda mfupi baada ya kujifungua

Akijua fika na baada pia ya kushauriwa na wataalamu faida ya maziwa ya mama amelibeba jukumu hilo kwa uaminifu licha ya changamoto kadhaa

Eagan Salla alimemtembelea mkoani Arusha wakati dunia ilipokuwa ikiadhimisha juma la unyonyeshaji na hii hapa taarifa yake