Magari ya zamani yampa kijana fursa ya kuishi ndoto yake

Maelezo ya video, Magari ya zamani yampa kijana fursa ya kuishi ndoto yake

Kijana wa Ktanzania Hussein Ngozi mwenye umri miaka 28 aliamua kuupiga teke ualimu aliosomea kwa takribani miaka mitatu na kuamua kujikita kwenye kufufua na kuyatengeneza magari ya zamani

Kwa kutumia pesa zake za mwisho za masomo ya elimu ya chuo kikuu Hussein alinunua gari aina ya Volkswageni beetle akinuia kuliweka kama kumbukumbu, lakini akiwa na gari hilo kwenye heka heka za kusaka ajira jijini Dar es salaam ndipo alipoiona fursa

Akiwa mkoani Iringa Mwandishi wa BBC Eagan Salla alizungumza naye na kuandaa taarifa ifuatayo