Anne-Marie alipoteza watoto wake wanne na mumewe wakati wa mauaji ya kimbari

Maelezo ya video, Anne-Marie alipoteza watoto wake wanne na mumewe wakati wa mauaji ya kimbari

Anne-Marie alipoteza watoto wake wanne na mumewe wakati wa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.Mwanaume mmoja kwa jina Celestin alivamia nyumbani kwa Anne-Marie na washambuliaji na kuwaua watoto wake wawili.

Washambuliaji walikua na marungu na mapanga.Celestin alichomoa panga na kukata shingo za watoto wawili.

Pamoja na aliyoyapitia Anne-Marie,Kasisi wa kikatoliki alimshawishi Anne-Marie kumsamehe Celestin.

Celestin amejutia dhambi aliyoifanya.