Mbilikimo waliteswa sana na Wabelgiji na wameendelea kuishi kijadi DRC
Kwenye kingo za Mto Congo, baadhi ya walioteswa zaidi na kufanyiwa unyama usioelezeka chini ya utawala wa Mfalme Leopold walikuwa ni watu wa jamii ya mbilikimo waliolazimishwa kuvuna raba kutoka kwenye miti msituni.
Mbilikimo bado huishi msituni wakiwinda wanyama, na kuchuma matunda ya porini.