Filamu ya Kitanzania yapaa anga za kimataifa

Maelezo ya video, Filamu ya Kitanzania kupaa anga za kimataifa

Sekta ya filamu imeendelea kukua kila kukicha nchini Tanzania,ambapo sasa filamu zinazotengenezwa nchini humo zinavuka anga ya kimataifa na kuonyeshwa sehemu nyingine duniani.

T Junction ni miongoni mwazo, na licha ya kwamba imeigizwa na vijana chipukizi lakini maudhui yake yameweza kugusa wengi.