Madonna ameanza ziara ya muziki huko Uingereza
Madonna amerejea kufanya ziara yake ya dunia ya Madame X huko London baada ya kuvunja tamasha la Portugal baada ya kile alichokitaja kuwa maumivu ya mwili. Nyota huyu wa kibao cha …Papa don’t preach…. alipanda jukwaani na kutumbuiza mashabiki wake japo alivaa vifaa vya kumsaidia kwenye magoti.
