Mtoto wa Kiswidi anayedumisha mila ya Wamasai

Maelezo ya video, Mtoto wa kiswidi atamani kuwa mmasai

Mtoto mwenye asili ya Uswidi (Sweden), Oscar Daudi ambaye mama yake ameolewa nchini Tanzania anapenda utamaduni wa kimasai na anajua kuongea kiswahili na kimasai.

Oscar mwenye umri wa miaka 11, anakaa Morogoro tangu akiwa na miaka saba.

Anatamani kuwa mfugaji na anajivunia utamaduni wa kimasai.

Yeye anavaa nguo za asili za kimasai peke yake.